Friday, 27 January 2017 00:07

RAIS TRUMP AIKAZIA MEXICO SASA BIDHAA ZAKE KUTOZWA KUTOZWA KODI MAREKANI


 
Ikulu ya Marekani imesema Rais wa nchi hiyo Donald Trump anaweza kutoza asilimia 20 ya kodi kwa bidhaa zinazoingizwa nchini humo kutoka Mexico kuweza kusaidia mpango wa kujenga ukuta kati ya nchi hizo mbili kuzuia kuingia kwa Wahamiaji haramu na madawa ya kulevya.

Mexico imesisitiza kuwa haitolipia gharama za ujenzi wa ukuta huo na kwamba pendekezo hilo jipya lililotolewa litasababisha kuzidisha ufa wa kidiplomasia kati ya nchi hizo mbili na kusababisha Rais Enrique Pena Nieto kufuta ziara yake ya kukutana na Rais Trump wiki ijayo mjini Washngton.
Uamuzi wa Rais Pena Nieto umeungwa mkono nchini mwake, akiwemo pia mtangulizi wake Vicente Fox.
Bwana Fox amesema ana uhakika Mexico italipiza kisasi kwa kutoza kodi bidhaa zitokazo Marekani, iwapo mipango hiyo ya Rais Trump itatimizwa.
Katika Hatua nyingine Waziri mkuu wa Uingereza Theresa May atakuwa kiongozi wa kwanza wa kigeni kukutana na Rais Trump.
Katika ziara yake nchini Marekani tayari amekutana na wanachama wa Republican mjini Philadelphia ambapo amesema Uingereza na Marekani hazipaswi kurudi katika kile alichokiita sera za uvamizi zilizoshindwa, walizokuwa wakizitumia awali.
Hata hivyo amesema nchi hizo mbili bado zina jukumu la kuongoza dunia

Thursday, 26 January 2017 23:57

SOKO LA MABOGA JUU KILOLO WENGI WALA MBEGU ZAKE KUONGEZA NGUVU ZA KIUME

BIASHARA ya maboga yenye mbegu yashika kasi katika migahawa Wilaya ya Kilolo mkoani Iringa baada ya baadhi ya wanaume kupenda kutumia maboga yenye Mbegu kwa ajili ya kuongeza nguvu za kiume.

Mtandao wa matukiodaimablog umebaini hali hiyo leo katika migahawa iliyopo nje ya ofisi ya Halmashauri ya Wilaya ya Kilolo kwa wanaume wanaofika kugombea maboga yenye mbegu kuliko vitafuno vingine.

Mfanyabiashara wa mgahawa eneo hilo Raha Juma Mlula anasema kuwa maboga yamekuwa yakiisha mapema kuliko maandazi ama vitafuno vingine na wateja wakikosa maboga husikitika zaidi.

Hata hivyo alisema kipande cha boga huuzwa Tsh 500 wakati chapati na maandazi ni Tsh 300 ila wengi hukimbilia maboga

Alisema boga moja kwa wakulima wananunua Tsh 1500 na wao hupata Tsh 3000 baada ya kuuza.

 Alisema kuwa kwa sasa upatikanaji maboga ni wa shida kutokana na watu wengi kupenda kutumia maboga wakati wa kunywa chai asubuhi.

" Wengi wanakula ni wanaume ambao wanaimani kuwa zinasaidia kuongeza nguvu za kiume…. Ila mimi najua mbegu za maboga zinazosaidia kuongeza nguvu za kiume au za kike ni zile mbichi zisizopikwa"

Habari zaidi utaipata baada ya kumpata mtaalam wa Afya